NA FRESHA KINASA
TIMU ya Biashara United Veteran imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya timu ya Musoma Veteran katika mchezo wa fainali uliochezwa katika Uwanja wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare Mjini Musoma ikiwa ni Maadhimisho ya Miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kabla ya mchezo huo wa fainali, ulichezwa mchezo wa kusaka mshindi wa tatu baina ya timu ya Chuo cha Uuguzi cha Musoma na timu ya Maendeleo ya Jamii Buhare. Ambapo timu ya Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare iliibuka kidedea kwa kushinda mikwaju ya penati 4-3.

Aidha, Binda amewaomba Watanzania kuendelea kudumisha amani, umoja, mshikamano na kushirikiana na serikali katika kuhakikisha Taifa linapiga hatua mbele za kimaendeleo.