Wanafunzi milioni 4 kunufaika kupitia Mradi wa Shule Bora nchini

*Bilioni 271/- kufanikisha utekelezaji wake katika mikoa tisa 

NA OR-TAMISEMI

SERIKALI ya Tanzania kwa ikishirikiana na Serikali ya Uingereza imezindua mpango wa elimu bunifu wa shule bora wenye thamani ya Shilingi bilioni 271 utakaosaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia, ujumuishi na usalama kwa wasichana na wavulana katika shule za msingi nchini.
Katika mpango huo, OR-TAMISEMI imeshirikiana pia na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, uzinduzi wa mradi huo umefanyika katika Shule ya Msingi ya Mkoani wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali akiwemo Naibu Waziri wa OR-TAMISEMI, David Silinde na Naibu Katibu Mkuu wa OR-TAMISEMI anayeshughulikia elimu, Gerald Mweli.
Wengine ni pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika, Vicky Ford, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, makatibu wa tawala wa mikoa ya Simiyu, Katavi, Kigoma, Tanga, Mara, Rukwa, Singida na Dodoma ambako mradi huo utatekelezwa. 

Akizungumza baada ya kuzindua mpango huo, Vicky amefurahia kwa kufanikishwa kwa mchakato huo, akisema ni mwanzo mzuri mpya wa ushirikiano katika sekta ya elimu kati ya Serikali ya Uingereza na Tanzania. Amesema, mradi huo utawanufaisha wanafunzi milioni 4 katika mikoa tisa.
"Mradi wa shule bora unakwenda pamoja na mfumo wa elimu wa Tanzania ili kuwasaidia wanafunzi na walimu katika kuwajengea uwezo.Mpango wa shule bora utatoa fursa hata kwa wale wanafunzi wenye mahitaji maalumu,"amesema Vicky. 

Kwa upande wake, Silinde amesema," jukumu langu ni kuishukuru Serikali ya Uingereza na tunakushuru Waziri (Vicky) kwa ujio wako Tanzania na hatua ya Serikali yako kutusaidia kwenye sekta ya elimu.

"Ahadi yetu ni fedha zote zitakazoletwa zitatumika malengo yaliyokusudiwa," amesema Silinde.

Naye, Profesa Mkenda amesema, mradi huo utatekelezwa katika mikoa tisa na utaboresha mazingira ya ufundishaji wa darasani pamoja kuwaendeleza walimu ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news