Waziri Dkt.Mabula awataka wanasiasa kuwa wakweli wanapotekeleza majukumu yao

NA MUNIR SHEMWETA-WANMM

WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt.Angeline Mabula amewataka wanasiasa nchini kuwa wakweli wakati wa kutekeleza majukumu yao ili kuepuka kuleta migongano baina ya Serikali na wananchi.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.Dkt Angeline Mabula akizungumza katika kikao kati ya Mawaziri wa Wizara za Kisekta na viongozi wa wilaya na mkoa wa Mbeya kuhusiana na utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975 Mei 6, 2022.

Dkt.Mabula ametoa kauli hiyo Mei 6, 2022 mkoani Mbeya wakati Kamati ya Mawaziri wa Wizara za Kisekta ilipokutana na uongozi wa mkoa na wilaya kwa lengo la kutoa mrejesho wa Maamuzi ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975.
‘’Tusitafute kura kwa kudanganya wananchi halafu mwisho wa siku tunakosa maneno mazuri ya kuwaambia kutokana na kuwaaminisha kuwa ukiwa kiongozi hawataondoka eneo fulani hivyo kupatwa na kigugumizi utaenda kusema nini wakati ushawaaminisha,"alisema Dkt.Mabula.

Sehemu ya washiriki wa kikao kati ya Mawaziri wa Wizara za Kisekta na viongozi wa wilaya na mkoa wa Mbeya kuhusiana na utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975 Mei 6, 2022. Naibu Waziri wa Kilimo Mhe.Anthony Mavunde akizungumza wakati wa kikao kati ya Mawaziri wa Wizara za Kisekta na viongozi wa wilaya na mkoa wa Mbeya kuhusiana na utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975 Mei 6, 2022.

Kwa mujibu wa Waziri Dkt Mabula, wanasiasa wanatakiwa kuwa wakweli kwenye masuala ambayo ni kwa ajili ya ulinzi, maendeleo na mustakabali wa nchi na kama kuna makosa yalifanyika huko nyuma kwa kusajiliwa vijiji maeneo ya hifsadhi basi wakaeleze ukweli na na kusisitiza serikali haiko tayari kurudia makosa.

Akigeukia uamuzi wa serikali kuhusu vijiji 975, Dkt Mabula alisema serikali ya mkoa wa Mbeya inalo jukumu la kusimamia utekelezaji wa uamuzi wa Baraza la Mawaziri kwa kushirikiana na taasisi na mamlaka zote zilizopo ndani ya mkoa.Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Mary Masanja akizungumza wakati wa kikao kati ya Mawaziri wa Wizara za Kisekta na viongozi wa wilaya na mkoa wa Mbeya kuhusiana na utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975 Mei 6, 2022.
Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Aweso akizungumza wakati wa kikao kati ya Mawaziri wa Wizara za Kisekta na viongozi wa wilaya na mkoa wa Mbeya kuhusiana na utekelezaji wa maamuzi ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975 Mei 6, 2022.

Mkoa wa Mbeya unahusisha vijiji/Mitaa 58 yenye migogoro ya matumizi ya ardhi ambapo vijiji 31 kati ya hivyo vitabaki kwenye maeneo yake huku vijiji/ mitaa 21 wataalamu wakifanyia tathmini na kutoa mapendekezo ya namna ya kutatua migogoro iliyopo kwa manufaa ya Taifa.

‘’Nitoe angalizo maeneo yote ambayo wataalam wanafanyia kazi serikali imekwisha chukua picha za anga za maeneo husika hivyo hatutegemei kuona shughuli mpya zikifanyika katika maeneo yote ambayo wataalam wanapita,’’ alisema Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news