NA DIRAMAKINI
JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia,BW.WARREN MAX MWINUKA (20) mkazi wa Makondeko Mbeya Mjini kwa tuhuma za kujifanya, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, JUMA ZUBERI HOMERA akitumia akaunti ya mtandao wa kijamii wa Instagram kwa jina la “juma_homera”.
JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia,BW.WARREN MAX MWINUKA (20) mkazi wa Makondeko Mbeya Mjini kwa tuhuma za kujifanya, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, JUMA ZUBERI HOMERA akitumia akaunti ya mtandao wa kijamii wa Instagram kwa jina la “juma_homera”.
"Mtuhumiwa alikuwa akitumia akaunti hiyo kuwaadaa watu kwa kujifanya ni Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na kutoa namba ya simu ya kwake ili wananchi waweze kutoa/kupeleka kero au shida mbalimbali kwake. Upelelezi wa shauri hili unaendelea na mara baada ya kukamilika atafikishwa mahakamani,"amesema.