Tunaipongeza Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa kuona umuhimu wa taasisi zake kushirikiana kiutendaji-Kamati

"Tunaipongeza Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa kuona umuhimu wa taasisi zake kushirikiana kiutendaji, ushirikiano ambao umetoa fursa kwa Watumishi Housing Investment kupewa kandarasi ya kujenga Chuo cha Utumishi wa Umma, Kampasi ya Singida, huu ni mfano mzuri wa kuigwa na taasisi nyingine,” Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mhe. Dennis Londo (Mb) amefafanua.

Ameongeza kuwa, kutokana na ufanisi wa kiutendaji wa WHI ni vema Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Serikali kwa ujumla kuona namna bora ya kuitumia taasisi hiyo katika ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja ujenzi wa nyumba kwa ajili ya makazi ya watumishi wa umma.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news