Mbunge Fredrick Lowassa afanya jambo Soko Kuu la Monduli

NA DIRAMAKINI

MBUNGE wa Jimbo la Monduli wilayani Monduli Mkoa wa Arusha, Fredrick Lowassa ametoa shilingi millioni 3.8 kwa ajili ya ukarabati wa paa la Soko Kuu la Monduli. 
Hayo yalijiri wakati wa ukaguzi wa miundombinu ya maendeleo ikiwemo barabara ya Monduli mjini inayojengwa kwa Kiwango cha lami ambapo wakati wa ukaguzi huo alisimamishwa na wafanyabiashara wa soko hilo na kutoa changamoto zao ikiwemo uchakavu wa soko hilo, na maji kujaaa ndani ya soko kipindi cha mvua.

Awali akizungumza mmoja wa wafanyabiashara katika soko hilo ambaye hakutaka kutajwa majina yake amesema changamoto yao kubwa ni miundombinu ya soko hilo, pamoja na kuomba kuondolewa kwa soko moja kwani wamekuwa wakimwaga vitu kutokana na kuharibika, kwani masoko yamekuwa mengi maarufu kama magulio.

Josephat Mbilinyi ni mwenyekiti wa soko hilo amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo pamoja na ukosefu wa mikopo zile asilimia kutoka halmashauri kwenda kwa wajasiriamali. 

Pia Mbunge Lowasa ametoa ahadi ya pikipiki 12 ambazo zitatolewa wiki ili ziweze kunufaisha kila kijiwe kilichopo Monduli Mjini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news