RITA yashiriki Nanenane Mbeya huku ikitoa vyeti vya kuzaliwa papo kwa papo

NA DIRAMAKINI

WAKALA wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) umewakaribisha wananchi wote kutembelea katika banda lao ili kupata huduma kwenye maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Wakulima yanayofanyika mkoani Mbeya katika viwanja vya John Mwakangale maarufu kama viwanja vya Nanenane.
Huduma zinazopatikana katika banda la RITA ni, Usajili wa vyeti vya kuzaliwa kwa watu wote waliozaliwa Tanzania bara, elimu kwa umma kuhusu usajili wa Ndoa na Talaka, Ufilisi na Udhamini pamoja na huduma ya msaada wa kisheria kuhusu masuala ya Wosia na Mirathi.
Akiongea kutoka viwanjani hapo, Afisa Usajili Msaidizi Bi. Noela G. Ituga anasema kuwa "tunapenda kuwakaribisha sana wananchi wote wafike katika banda letu ili kufaidika na huduma zetu kwa urahisi kabisa ambapo pia tunasajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa hapahapa viwanjani kwa kila mtu aliyezaliwa ndani ya mipaka ya Tanzania bara hivyo basi wakulima na watanzania wote wasiokuwa na vyeti hivi muhimu watembelee katika banda la RITA kupata huduma zetu".
Maonesho hayo yaliyoanza Agosti Mosi yanatarajiwa kufikia kilele Agosti 8, 2022 ambapo kitaifa yanafanyika katika viwanja vya John Mwakangale maarufu viwanja vya Nanenane mkoani Mbeya na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news