Wajane wazidi kuunganisha nguvu kupitia chama chao cha CCWWT

NA DIRAMAKINI

WANAWAKE wajane wameendelea kuunganisha nguvu ya pamoja kupitia chama chao, Chama cha Wanawake Wajane Tanzania (CCWWT) kuanzia ngazi za chini hadi Taifa.
Lengo la kufanya hivyo ni kuunganisha nguvu ya pamoja ili kutambuana, kufahamiana, kujua changamoto mbalimbali waanazopitia kila mmoja ambapo kwa umoja wao wanaweza kuzipatia ufumbuzi wa kimawazo au kuwezeshana kadri inavyowezekana.

Hayo yamebainika Agosti 12, 2022 baada ya Mwenyekiti wa CCWWT Taifa,Bi.Rabia Ally Moyo kushiriki katika uzinduzi wa chama hicho tawi la Tandale kwa Tumbo lililopo Kata ya Tandale ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Bi.Moyo amebainisha kuwa, umoja ni nguvu kubwa kwa wajane ambao utawawezesha kuibua mambo mbalimbali wanayokabiliana nayo katika maisha ya kila siku ikiwemo kijamii, kiuchumi na mengineno ambapo baada ya kuyachakata watafahamu wapi pa kuanzia ili kuyapatia ufumbuzi.

Amesema, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan inawathamini ndiyo maana aliunda wizara ambayo pamoja na mambo mengine, kundi la wajane limetajwa kama sehemu ya kusimamiwa na wizara hiyo.
Ni Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ambayo inaongozwa na Waziri, Mheshimiwa Dkt.Dorothy Gwajima huku akiwa mstari wa mbele kuwasikiliza, kuwashauri na hata kuyapatia ufumbuzi mahitaji ya wanawake wajane nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news