Watafiti wa TARI kuja na mwarobaini wa kumdhibiti Funza wa Vitumba

NA MWANDISHI WETU

IMEELEZWA kuwa, Funza wa Vitumba ni tishio kwa mazao mengi kutokana na kwamba anaanza kushambulia mazao pale yanapoanza kutoa maua.

Hayo yamesemwa na Mtafiti wa Wadudu waharibifu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Ukiriguru, Romana Cornel kwenye Maonesho ya Nane Nane yanayoendela katika viwanja vya Nyamhongolo jijini Mwanza.
Amesema Funza wa Vitumba ni hatari kwani anaanza kushambulia mazao pale yanapoanza kutoa maua.

“Kwa upande wa pamba ni wiki ya nane lakini pia anaharibu mazao mengine, anashambulia mahindi na kama unavyoona hawa tumewatoa kwenye dengu na mtama pia wanashambulia. Ni vyema wakulima wakatumia mitego hii kuwatega. Watumie mabaki ya Sukari yaani Molases na huu mtego tuliouweka hapa na tumeweka juu yake harua, hapa vipepeo dume wote wamenaswa. Hivyo vipepeo majike hawataweza kutaga mayai”, amesema mtafiti huyo.

“Kwa sasa bado tupo kwenye utafiti wa njia nzuri zaidi kupambana na wadudu hawa na mwaka ujao matokeo yatakuwa tayari hivyo itakuwa ni nafuu kwa wakulima kwani funza huyu atakuwa amepatiwa suluhisho,”amesema Cornel.

Funza wa vitumba anachukuliwa kuwa mmoja kati ya wadudu wasumbufu muhimu zaidi duniani kote, wanaoshambulia zaidi ya aina 200 za mimea.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news