Waziri Mkuu afungua Mkutano Mkuu wa CAF jijini Arusha

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya washirki wa Mkutano Mkuu wa 44 wa Shirkisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Cha Arusha (AICC), Agosti 10, 2022. Wa nne kushoto ni Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohammed Mchengerwa na wa tatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongela.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozana na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) Dkt. Patrice Motsepe (kulia) na Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo , Mohammed Mchengerwa (kushoto) wakati alipoingia Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha, ( AICC) kufungua Mkutano Mkuu wa 44 wa CAF, Agosti 10, 2022. Wa Pili kulia ni Rais wa Shirkikisho la Soka Duniani (FIFA), Gianniu Infantino.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishiriki kuimba Wimbo wa Taifa kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa 44 wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Agosti 10, 2022. Kushoto ni Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani, Gianniu Infantino na wa watatu kushoto ni Rais wa Shirkikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF), Patrice Motsepe.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Mkutano Mkuu wa 44 wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC). Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea zawadi ya nembo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) kutoka kwa Rais wa Shirikisho hilo, Dkt. Patrice Motsepe baada ya kufungua Mkutano Mkuu wa 44 wa CAF kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).
Baadhi ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa 44 wa Shirkikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipofungua mkutano huo kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Agosti 10, 2022. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news