HITILAFU YA UMEME KATIKA MTAMBO WA UZALISHAJI MAJI RUVU CHINI

NA DIRAMAKINI

MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawatangazia Wateja na wananchi wanaohudumiwa na mtambo wa kuzalisha maji Ruvu Chini kuwa kumekuwa na ukosefu wa maji kutokana na changamoto ya umeme iliyojitokeza kuanzia asubuhi ya tarehe 27.09.2022.
Hitilafu hiyo imesababisha mtambo kutoweza kufanya kazi hivyo kupelekea upungufu wa huduma ya maji katika mji wa Bagamoyo na sehemu kubwa ya mkoa wa Dar es salaam.

Maeneo yanayoathirika ni pamoja na; Bagamoyo, Mapinga, Mabwepande, Bunju, Tegeta, Mbweni, Boko, Salasala, Kunduchi, Mbezi Beach, Goba, Mivumoni, Madale, Kawe, Lugalo, Makongo, Chuo Kikuu, Mwenge, Kijitonyama, Mikocheni, Msasani, Oysterbay, Masaki, Mwananyamala, Kinondoni, Magomeni, Kigogo, Chang'ombe, Keko, Kurasini, Kigamboni, Airport, Kiwalani, Buguruni, Vingunguti, Ilala na Katikati ya mji.

Mafundi wa TANESCO wanaendelea na jitihada kuhakikisha huduma ya umeme inarejea.

Wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (bure) au
0735 202-121(WhatsApp tu)


Tovuti: www.dawasa.go.tz
Mitandao ya kijamii.

Facebook: https://www.facebook.com/pg/Dawasaofficial/posts/
Instagram: https://instagram.com/dawasatz?utm_medium=copy_link

Twitter: https://twitter.com/dawasatz?s=08
YouTube: https://youtube.com/channel/UCCVyHKIvUwDFG1tUyWhd7fQ

Imetolewa na 

Kitengo cha Mawasiliano na Jamii

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news