Rais Samia awataka Mawakili wa Serikali kutoa elimu kwa umma

NA DIRAMAKINI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemuagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupitia upya Sheria za uwekezaji pamoja na biashara nchini ili kukabiliana na migogoro inayotokana na Sheria hizo.
Rais Samia ametoa agizo hilo Septemba 29,2022 wakati akizindua Chama cha Mawakili wa Serikali katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete.
Aidha, Rais Samia amesema ni vyema Mawakili wa Serikali wawe makini na kuharakisha kusikiliza migogoro inayokinzana na Sheria za uwekezaji ili kupunguza kupelekana Mahakamani na wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa nchini.

Rais Samia amesema kufanya hivyo kutasaidia kupunguza kesi za uwekezaji, kulinda uwekezaji nchini na kupanua wigo wa kukuza uwekezaji, kukusanya mapato na hivyo kukuza uchumi kwa maslahi ya taifa.
Kwa upande mwingine, Rais Samia amewataka Mawakili wa Serikali kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu bila kukiuka haki za wananchi na kuwasaidia kutatua kero zao ambazo hazihitaji kufikishwa mahakamani.
Rais Samia pia ametoa wito kwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu pamoja na Mawakili wote wa Serikali kuendelea kutoa elimu kwa umma hususan sheria zinazowagusa wananchi na kuwaelekeza taratibu za namna ya kupata haki zao.

Vile vile, Rais Samia amesema utoaji wa elimu utapunguza mrundikano wa mashauri ambayo hayana ulazima wa kufikishwa mahakamani kwa ajili ya utatuzi na hivyo pia kuchangia kupunguza mrundikano wa mahabusu.
Rais Samia amewataka Wakuu wa Mikoa kutumia Kamati za Ushauri wa Kisheria zilizoanzishwa katika ngazi zote za Mikoa na Wilaya nchini kupunguza malalamiko ya wananchi na mashauri dhidi ya Serikali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news