Mhe.Silinde:Kijiji chochote nchini hakitasajiliwa bila kushirikisha wizara za kisekta

NA MWANDISHI WETU

NAIBU Waziri wa Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Mhe.David Silinde (Mb) amesema Serikali imetoa agizo kwamba kwa Mikoa na Halmashauri zisisajili kijiji chochote au maeneo mapya ya utawala bila kushirikiana na Wizara nyingine za kisekta.
Ameyasema hayo Oktoba 12, 2022 mkoani Katavi wakati wa Ziara ya Mawaziri wa Kisekta ya kutatua migogoro ya Ardhi katika vijiji 975 nchini.
"Hatutasajili hayo maeneo mpaka kuwepo na ushauri au mapendekezo kutoka kwa Wizara za Kisekta kama Maliasili, Ardhi na nyinginezo," Mhe. Silinde amesisitiza.
Amefafanua kuwa lengo la Serikali ni kuondokana na changamoto za migogoro ya ardhi zinazoendelea kujitokeza nchini.Ziara ya Kamati ya Mawaziri wa Kisekta itaendelea katika mkoa wa Geita.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news