WAZIRI MKUU AENDA KOREA KUSINI KWA ZIARA YA KIKAZI

NA MWANDISHI WETU

WAZIRI MKUU wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa ameondoka nchini leo Jumapili, Oktoba 23, 2022 kwenda  jijini Seoul, Jamhuri ya Korea kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu.
Akiwa Korea Kusini, Mheshimiwa Majaliwa atakutana na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Mheshimiwa Han Duck-soo. Pia anatarajiwa kushiriki kongamano la biashara na kukutana na wamiliki wa makampuni makubwa na wenye viwanda. Vilevile, atakutana na Watanzania waishio Korea Kusini.

Kupitia vikao hivyo, Tanzania inatarajiwa kuimarisha mahusiano na Korea Kusini ambayo yamedumu kwa miaka 30. 

Vilevile, kukuza mahusiano ya kibiashara na uwekezaji, kuangalia fursa za kukuza uchumi wa bluu, utalii, mahusiano ya anga na ushirikiano kwenye sekta ya sanaa na utamaduni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news