Yanga SC yatinga hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika

NA DIRAMAKINI

YANGA SC ambao ni Mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara wametinga hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.
Ni baada ya kuichapa bao 1-0 wenyeji Club Africain kupitia mchezo uliopigwa katika dimba la Le stade olympique de Radès jijini Tunis nchini Tunisia leo Novemba 9, 2022.

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Yanga, Stephane Aziz Ki ndiye shujaa wa klabu hiyo ambapo akitokea benchi aliipatia bao muhimu timu yake dakika ya 79 akimalizia pasi ya Fiston Mayele.

Awali dakika 45 zilitamatika kwa timu zote mbili ubao kusoma sufuri, baada ya miamba hiyo kuoneshana soka la hali ya juu.

Katika mtanange huo, Kibwana Shomari ni miongoni mwa wazawa ambao wameonesha kiwango kizuri kwenye mchezo akiwa amepiga mashuti mawili ambayo yamelenga lango.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news