Shirika la Reli Tanzania (TRC) laongeza mabehewa mapya 22 kuongeza ufanisi

NA DIRAMAKINI

SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) limeanza kufanya majaribio ya mabehewa mapya 22 yaliyonunuliwa na Serikali kwa ajili ya reli ya kati na Kaskazini ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma zake kwa wananchi.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Desemba 11, 2022 na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa shirika hilo, Jamila Mbarouk.

Bi.Mbarouk amesema kuwa,majaribio ya mabehewa hayo yameanza kwa kuyasafirisha umbali wa kilomita 400 kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro huku ukiwepo pia mpango wa kuyafanyia majaribio kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma na Arusha.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news