Majambazi yakutwa na AK47, mabomu mkoani Kagera

NA DIRAMAKINI

JESHI la Polisi mkoani Kagera limewaua watu wawili wanaosadikiwa kuwa ni majambazi katika Kijiji cha Kumunazi wilayani Ngara mkoani humo.

Kamanda wa Polisi Mkoa Kagera, William Mwampaghale amesema, watuhumiwa hao wanakadiriwa kuwa na umri wa miaka 25 na 30, lakini majina yao bado hayajatambulika, ila miili imehifadhiwa Hospitali ya Rufaa ya Nyamihaga wilayani Ngara.

Amesema, Januari 21, 2023, polisi walipata taarifa kuwa kuna kundi la wahalifu wanaotumia pikipiki linapanga kufanya uhalifu kati ya barabaraba ya Kumunazi na Rulenge, ambapo majira ya saa 3:35 polisi liliweka mitego mbalimbali na kufanikiwa kunasa wahalifu hao, ambao walikufa katika kurushiana risasi.

Kamanda Mwampaghale amesema, katika mtego wao ilipita pikipiki waliyoihofia ambayo ilikuwa imebeba watu watatu,polisi waliisimamisha pikipiki hiyo lakini haikusimama, wakafyatua risasi juu, lakini bado waliendelea kukimbia.

Amesema, waliwakimbiza lakini walikaidi na kuanza kurushiana risasi, ambapo mmoja alijeruhiwa mguuni na mwingine kiunoni na hali zao zilikuwa mbaya wakati wakikimbizwa Hospitali ya Nyamihaga.

Hata hivyo, amesema, mara baada ya kufanya upekuzi kwenye makoti waliyokuwa wamevaa, walikutwa wakiwa wamebeba bunduki aina ya AK47, ikiwa na risasi 25 pamoja na mabomu mawili ya kurusha kwa mkono.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news