Kenya, Eritrea zafungua ukurasa mpya

NA DIRAMAKINI

JAMHURI ya Kenya na Eritrea zimekubali kufuta kabisa mahitaji ya visa kwa raia wao ili kuchochea kasi ya ukuaji wa kiuchumi baina ya pande mbili hizo.

Eritrea, nchi ya Pembe ya Afrika, iliyoko kwenye Bahari Nyekundu. Eneo la pwani la Eritrea limekuwa muhimu kwa muda mrefu katika historia na utamaduni wake, jambo ambalo limeakisiwa katika jina lake, ambalo ni toleo la Kiitaliano la Mare Erythraeum, Kilatini ikimaanisha Bahari Nyekundu.

Bahari Nyekundu ndiyo njia ambayo Ukristo na Uislamu ulipitia eneo hilo, na ilikuwa njia muhimu ya kibiashara ambayo mataifa yenye nguvu kama Uturuki, Misri, na Italia yalitarajia kutawala kwa kunyakua udhibiti wa bandari kwenye pwani ya Eritrea.
Picha na Ikulu.

Tangazo hilo lilitolewa Alhamisi iliyopita katika Ikulu ya Nairobi, wakati Rais William Samoei arap Ruto alipofanya mazungumzo ya pande mbili na mwenzake wa Eritrea, Isaias Afwerki.

"Lazima tuwe na utawala usio na vikwazo vya kuunganishwa zaidi, kuimarisha mawasiliano na kuimarisha biashara ya kikanda,"alisema Rais Ruto.
Nchi hizo mbili zilikubaliana kuwa, kuna uwezekano mkubwa wa biashara na uwekezaji kati yao ambao unahitaji ushirikiano uliopangwa na ukapangika.

Walitaja nishati mbadala, usimamizi wa maji, kilimo, usafiri, ulinzi, utalii, madini, michezo, uchumi wa bluu na elimu kuwa ni mambo muhimu.

Kufikia 2020, kiwango cha biashara kati ya Kenya na Eritrea kilifikia shilingi milioni 73.4 ikilinganishwa na shilingi milioni 257 mwaka 2015. Rais Ruto alisema idadi hiyo ya chini ni kiashiria kwamba fursa katika biashara ni kubwa.
"Pamoja na ufanyaji kazi wa Eneo Huria la Biashara Huria la Bara la Afrika, ni lazima tushirikiane katika kupanga maeneo yenye manufaa ya kiuchumi kwa nchi zetu,"alisema Rais Ruto huku akipongeza kwa kujitolea kwa Eritrea katika kudumisha amani na utulivu katika eneo hilo.

Mheshimiwa Rais Ruto alibainisha kuwa, hatua hiyo imefungua njia ya ushirikiano kwa amani na maendeleo ya kikanda.

Rais Afwerki alisema Eritrea imejitolea kuchukua hatua zitakazowezesha kuimarika kwa uhusiano wa kiuchumi, kijamii na kiutamaduni na Kenya.

"Tutaendelea kukuza uwekezaji wa pamoja na kufanya kazi pamoja katika kuimarisha amani na usalama endelevu," alisema wakati wa mkutano wao wa pamoja na vyombo vya habari jijini humo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news