Dhoruba kubwa ndani ya Ziwa Victoria yasababisha uharibifu wa mitumbwi na nyavu,Mbunge Prof.Muhongo atoa ombi

NA FRESHA KINASA

MBUNGE wa Jimbo la Musoma Vijijini mkoani Mara, Prof. Sospeter Muhongo ametoa wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia ikiwemo kuwachangia wavuvi wa jimbo hilo walioharibiwa mitumbwi na makokoro yao kufuatia dhoruba ya mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali.
Juzi, Machi 20, 2023 upepo wenye kasi kubwa na mvua kubwa vilisababisha kuwepo kwa dhoruba kubwa ndani ya Ziwa Victoria.Mialo ya Musoma Vijijini ilikumbwa na dhoruba hiyo na uharibifu mkubwa umefanyika. 

"Tunaomba tushirikiane kuwachangia wavuvi wetu walioathirika na janga hili. Tathimini ya uharibifu huu inaonesha kuwa,mitumbwi ya Mwalo wa Kijiji cha Busekera iliyoharibika ni 137, inayotengenezeka ni 108,isiyotengenezeka ni 29.
"Aidha, makokoro ya dagaa yaliyoharibika ni 29, mitumbwi ya Mwalo wa Kijiji cha Buira iliyoharibika ni 39, inayotengenezeka ni 29,isiyotengenezeka ni 10 na makokoro ya dagaa yaliyoharibiwa ni 15,"amefafanua Mbunge Prof.Muhongo kupitia taarifa iliyotolewa leo Machi 22, 2023.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mitumbwi ya Mwalo wa Kijiji cha Bwai Kumsoma iliyoharibika ni 25, inayotengenezeka ni 21, isiyotengenezeka ninne huku makokoro ya dagaa yaliyoharibika yakiwa ni 15.
Aidha, kwa upande wa mitumbwi ya Mwalo wa Kijiji cha Kasoma tathimni inaonesha kuwa, iliyoharibika ni 10,inayotengenezeka ni tisa,isiyotengenezeka ni moja huku makokoro ya dagaa yaliyoharibika yakiwa ni matatu.

Wakati huo huo, grahama za matengenezo tathimini inaonesha kama ilivyo mifano ya hapa chini ambayo inakupatia picha unayoweza kuitumia kutoa mchango wako;

(1) Gharama za kutengeneza Mtumbwi

Tsh 1,700,000

Ubao 1 wa 9"x10"

Tsh 12,000

(2) Gharama za kutengeneza Kokoro la Dagaa

Tsh 1,400,000

UWASILISHAJI WA MCHANGO WAKO

Tafadhali mpelekee:

DC Wilaya ya Musoma

Simu: 0756 088 624

Michango ya awali:

Kwa mujibu wa taarifa hiyo,wataanza kuwasilisha michango ya awali kwa wavuvi waathirika siku ya Alhamisi ya Machi 30,2023.
Baadhi ya picha zinaonesha sehemu ndogo ya uharibifu uliofanyika kwenye Mwalo wa Kijiji cha Busekera, Kata ya Bukumi, Musoma Vijijini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news