Dkt.Kikwete awapa neno wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania jijini Seoul

NA MWANDISHI WETU

RAIS mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Jakaya Kikwete ametembelea Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Seoul, Korea Kusini na kuzungumza na wafanyakazi. 
Akiwa na mwenyeji wake Balozi Togolani Mavura, Dkt.Kikwete amewahimiza kuendelea kuchapa kazi kwa bidii na kuunga mkono kazi kubwa inayofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Kimataifa inayoshughulikia Masuala ya Elimu Duniani (Global Partnership for Education) - GPE) yuko Seoul, Korea Kusini kwa ajili ya kukutana na viongozi wa Serikali na mashirika Mbalimbali ya Korea Kusini.
Lengo la kukutana na viongozi wa Serikali na mashirika ni kwa ajili ya kujadili mikakati ya kuendelea kuboresha elimu katika nchi zinazoendelea. 

GPE ambayo ilianzishwa na nchi za G7 miaka 20 iliyopita, imeendelea kupigania elimu kwa ajili ya mtoto wa kike na wa kiume kwa kuomba kuungwa mkono na nchi na taasisi zinazoweza kuchangia katika elimu duniani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news