Kipindi Maalum: Ziara ya Waziri Mkuu nchini Urusi kushiriki Mkutano wa Russia-Africa Summit

JAMHURI ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Shirikisho la Urusi zina mahusiano mema zaidi ya kidiplomasia ambayo yameendelea kuwa na manufaa bora zaidi kwa ustawi wa pande zote mbili.

Pande hizo zimekuwa zikijikita zaidi katika kuendeleza na kufungua maeneo mapya ya ushirikiano katika sekta mbalimbali kwa maslahi mapana ya mataifa hayo.

Julai 27,2023 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alihudhuria Mkutano wa Pili wa Kilele baina ya Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka mataifa ya Afrika na Urusi uliofanyika Kituo cha Mikutano na Maonesho Expo Forum, St. Petersburg nchini Urusi akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo.

Ofisi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inakuletea Kipindi Maalum cha Ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa nchini Urusi kushiriki Mkutano wa Russia-Africa Summit. Endelea;

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news