DAR ES SALAAM-Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila amepongeza Wakala wa Mabasi yaendayo haraka (DART) kwa kutumia mfumo wa kudhibiti kugushi tiketi (msimbo code) na kuanza mchakato wa matumizi ya kadi maalum kwa wateja wake.
![](https://www.tamisemi.go.tz/storage/app/uploads/public/64c/3c6/d78/thumb_4214_800_420_0_0_auto.jpg)
Naye Mtendaji Mkuu wa DART, Dkt. Edwin Mhede amesema, Dart ina mpango wa kuanza rasmi matumizi ya kadi mapema baada ya mwezi Machi, mwakani.
"Tayari kadi zimekwishanunuliwa na mchakato wa kufunga mfumo wa kadi unaendelea na mwezi Machi utaanza kuwekwa kwenye mageti,"amesema.
Pia, amesema DART inatarajia kuanza safari kutoka Mbagala hadi Gerezani mapema mwezi Machi, 2024.
Tags
Dar es Salaam Region
Habari
Ofisi ya Rais-TAMISEMI
OR TAMISEMI
OR-TAMISEMI
TAMISEMI
Wakala ya Mabasi Yaendayo Haraka (DART)