🔴LIVE:Rais Dkt.Samia akishiriki Kilele cha Mbio za mwenge wa Uhuru na Kumbukumbu ya Baba wa Taifa

MANYARA-Hayati Baba wa Taifa , Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alizaliwa Aprili 13, mwaka 1922 katika kijiji cha Butiama Wilaya ya Musoma, Mkoa wa Mara, Tanzania (wakati ule ilikuwa Tanganyika).

Kila ifikapo Oktoba 14 huwa ni kumbukizi ya kifo chake ambapo leo Oktoba 14, 20023 anafikisha miaka 24 tangu atangulie mbele za haki huku Taifa na vizazi vyake vikiendelea na kumbukumbu ya kifo chake na kumuenzi.

Kitaifa Maadhimisho hayo huambatana na sherehe za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Mgeni rasmi anakuwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki Kilele cha Mbio za mwenge wa Uhuru na Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Baba Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Wiki ya Vijana kitaifa katika Uwanja wa Kwaraa Babati, Mkoani Manyara leo tarehe 14 Oktoba, 2023

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news