ADC YATOA WITO KWA WATANZANIA KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA NHIF

TANGA-Katibu Mkuu wa Alliance for Democratic Change (ADC) Dira ya Mabadiliko,Doyo Hassan Doyo ametoa wito kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Bima ya Afya nchini (NHIF) ili kukidhi mahitaji ya kujihudumia kiafya kwani kufanya hivyo kutasaidia wananchi wengi kupata huduma ya afya kwa urahisi zaidi na kwa ufanisi.
Ametoa wito huo leo jijini Tanga alipokuwa anazungumza na wanahabari katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo.

Doyo ameyasema hayo baada ya kutakiwa kutoa maoni yake juu ya uboreshaji wa huduma za afya hapa nchini.

Aidha,ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa namna inavyoboresha huduma za afya kote nchini, pamoja na hayo Doyo ameiomba serikali kuangalia upya sera yake ya afya ya kuchangia vifaa, huduma tiba kabla ya huduma ili kumsaidia mtanzania kuwahi kupata huduma na baada ya huduma ndugu wa mgonjwa waweze kufanya malipo.

Doyo amesema,kwa kufanya hivyo kutarahisisha matibabu ya wagonjwa na kuwanusuru na mateso ya ugonjwa wakati wakisubiria malipo yafanyike ndipo wapate tiba.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news