Mwajiriwa wa TCCIA Manyara achagua kulipa faini tuhuma za kughushi nyaraka

MANYARA-Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara imemhukumu, Ramadhani Rashid Msangi ambaye aliwahi kuwa Mshauri wa Wafanyabiashara mwajiriwa wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) mkoani Manyara.
Ramadhani ameamriwa kulipa faini kiasi cha shilingi 900,000 au kwenda jela miaka mitatu, kwa kosa la kughushi nyaraka za malipo.

Hukumu hiyo dhidi ya Ramadhani Rashid Msangi katika shauri la uhujumu uchumi Na. 05/2023, imetolewa Machi 22,2024 chini ya Mhe. Martin Massao, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Manyara.

Ilidaiwa mshtakiwa alighushi nyaraka mbalimbali katika marejesho yake kuonesha kuwa alihudhuria na kuendesha mafunzo ya wajasiriamali yaliyofanyika wilayani Hana'ng kwa kipindi cha mwezi Februari na Juni mwaka 2018.

Katika kipindi hicho inadaiwa alitumia kiasi cha shilingi 6,695,000 kugharamia posho ya chakula, ukumbi na nauli kwa waliodaiwa kushiriki mafunzo hayo huku akijua taarifa hizo hazikuwa sahihi.

Aidha,mshitakiwa amelipa faini na kuachiwa huru na Mahakama.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news