Tanzania,Kenya zakubaliana kuondoa vikwazo vya kibiashara visivyo vya kiushuru

KISUMU-Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Kenya zimekubaliana na kutia saini makubaliano ya kuondoa vikwazo vya kibiashara visivyo vya kiushuru ili kuruhusu raia kutoka nchi hizo kufanya biashara baina yao kwa urahisi na kwa manufaa ya pande zote mbili. Makubaliano hayo yametiwa saini na Wakili Stephen Byabato Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa na mwenzake Mhe. Rebbecca Miano, Waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda kutoka nchini Kenya. Makubaliano hayo yamefikiwa wakati wa Mkutano wa nane (8) wa Kamati ya Pamoja ya Biashara baina ya Tanzania na Kenya katika ngazi ya Mawaziri uliofanyika Kisumu nchini Kenya tarehe 22/03/2024.
Mkutano huo ulianza kwa ngazi ya watalaam kisha ngazi ya Makatibu Wakuu ambapo zaidi ya vikwazo vya kibiashara visivyo vya kiushuru zaidi ya 14 vilijadiliwa na kuwekewa mpango wa kuendelea kuviondoa vyote.
Tanzania na Kenya ni wabia wakubwa wa biashara na hivyo kuondolewa kwa vikwazo hivyo vitasaidia kuongezeka mara dufu kiwango cha kufanyika kwa biashara baina ya mataifa hayo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news