Kamati Tendaji ya Utafiti wa Sekta ya Utalii Tanzania (TTSS) yafanya kikao cha kawaida

DAR ES SALAAM-Aprili 4,2024 Kamati Tendaji ya Utafiti wa Sekta ya Utalii Tanzania (TTSS) imefanya kikao chake cha kawaida Ofisi ya Makao Makuu Ndogo ya Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Kikao hicho chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbas na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba, kinawashirikisha wajumbe kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Bodi ya Utalii Tanzania, Ofisi ya Uhamiaji, Ofisi ya Takwimu ya Taifa na Benki Kuu ya Tanzania.
Kikao kimejadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya utalii kwa ujumla, ikiwa ni pamoja wasilisho la matokeo ya utafiti wa wageni wa kimataifa waliotembelea Tanzania mwaka 2023.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news