MORONI-Kampuni za Kitanzania zimetakiwa kuomba kandarasi za ujenzi wa miradi inayofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Ufaransa visiwani Comoro.
Hayo yameelezwa wakati wa mazunguzo kati ya Balozi wa Tanzania, Comoro, Mhe. Saidi Yakubu na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa, Comoro, Bi.Rejane Hugouneno De Vreyer yaliyofanyika Moroni Machi 12, 2025.


Kwa upande wake, Balozi Yakubu alimweleza Bi De Vreyer kuwa Tanzania ina ushirikiano mkubwa na Comoro katika maeneo yote aliyoyazungumzia na kwa hivi sasa wamekwishaanza kualika kampuni za Kitanzania kuchangamkia fursa za zabuni zinazotangazwa visiwani Comoro.