DAR-Klabu ya soka ya Yanga, imekiri kupokea barua ya majibu kutoka CAS kuhusu kesi yao yenye namba CAS 2025/1/11298 ikiwataka warudi kwenye Kamati za ndani za Soka kabla ya kurudi tena CAS, lakini hata hivyo, wamesema wao hawapo tayari kurudi katika kamati hizo.
Yanga wamesema, hawawezi kurudi kwenye Kamati za ndani wakidai zina uonevu, uvunjwaji mkubwa wa kanuni na upendeleo wa dhahiri kwa baadhi ya timu.
Kama hiyo haitoshi, Yanga wamesema msimamo wao upo palepale kwamba hawatacheza mchezo namba 184 dhidi ya Simba.