DODOMA-Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja ametembelea jengo jipya la ofisi za Wizara ya Fedha lililopo Mji wa Serikali-Mtumba mkoani Dodoma.
Katika ziara hiyo,msimamizi wa ujenzi upande wa Mkandarasi, Bw. Govind Vaghjiyani, alimtembeza katika ofisi mbalimbali za viongozi,wakuu wa idara na vitengo na kujionea kazi kubwa iliyofikiwa katika ujenzi wa jengo hilo ambalo ni “State of the Art”.
