BoT yaungana na wadau mbalimbali kutoa elimu Maonesho ya Utalii ya Karibu-Kilifair 2025

ARUSHA-Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeungana na wadau mbalimbali wa sekta ya utalii kushiriki Maonesho ya Utalii ya Karibu-Kilifair 2025, yanayofanyika katika viwanja vya Magereza, jijini Arusha kuanzia tarehe 06 hadi 08 Juni.
Kupitia ushiriki huu, Benki Kuu inatumia fursa hiyo kutoa elimu kwa umma kuhusu majukumu yake ya msingi katika kusimamia uchumi nchini.
Katika maonesho hayo, Benki Kuu imeweka msisitizo maalum kwenye Kanuni za Matumizi ya Fedha za Kigeni za Mwaka 2025, ambazo zinalenga kuimarisha uthabiti wa thamani ya Shilingi ya Tanzania ili kuchochea maendeleo endelevu ya uchumi na kuhakikisha ustawi wa taifa kwa ujumla.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news