Mwenyekiti mstaafu kizimbani kwa rushwa

MBEYA-Katika Mahakama ya Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya, mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Neema Christopher, imefunguliwa shauri la jinai namba 14859/2025, Jamhuri dhidi ya Mwenyekiti wa Kijiji cha Lualaje Bw. Matatizo Kubelo Mwambipile.
Mshtakiwa anashtakiwa kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa chini ya kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.

Mshtakiwa alikuwa ni mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya katika nafasi ya Mwenyekiti wa Kijiji cha Lualaje kilichopo Kata ya Lualaje

Akisoma hati ya mashtaka, Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU,Kissa Ngoloke, Juni 18, 2025 alisema mshtakiwa aliomba na kupokea rushwa ya kiasi cha sh.800,000 ili aweze kumsaidia mwanakijiji mmoja kumpatia sehemu ya shamba la kijiji, hivyo kuisababishia hasara halmashauri hiyo kiasi cha shilingi 800,000.

Mshtakiwa amekubali kutenda kosa hilo na kutiwa hatiani na kuhukumiwa kulipa faini ya 500,000 au kutumikia kifungo cha miaka 3 jela.

Pia ameamriwa kurejesha sh.800,000 aliyopokea kwa njia za rushwa. Mshtakiwa amelipa faini ya sh.500,000 na amerejesha sh. 800,000.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news