Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuwekeza katika michezo-Waziri Mkuu

DAR-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Juni 01, 2025 amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan katika tuzo za wanamichezo waliofanya vizuri katika mashindano ya kimataifa zinazoandaliwa na Baraza la Michezo Taifa (BMT).
Lengo la tuzo  hizo ambazo zitafanyika katika Ukumbi wa Superdome uliopo Masaki jijini Dar es Salaam ni kuwaenzi na kuwatambua watanzania wanaiowakilisha nchi katika michezo mbalimbali duniani na kuiletea sifa Tanzania kwa maslahi yao na Taifa kwa ujumla.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali ya awamu ya Sita itaendelea kuwekeza katika sekta ya michezo kwa kuwa inatambua michezo ni afya, ajira, mshikamano, maendeleo lakini pia michezo ni burudani.

Katika hafla hiyo Mheshimiwa Majaliwa alipokea kwa niaba ya Rais Dkt. Samia tuzo ya kutambua mchango wake katika kukuza na kuendeleza sekta ya michezo nchini.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa pia alikabidhiwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kusimamia michezo nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news