TFS yaendelea kusisitiza misingi ya utawala bora mahala pa kazi kwa wahifadhi

IRINGA-Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeendelea kuimarisha misingi ya utawala bora kwa watumishi wake kwa kutoa mafunzo ya mara kwa mara yanayolenga kuongeza uadilifu, uwajibikaji na kupambana na vitendo vya rushwa katika maeneo ya kazi.
Katika muendelezo wa juhudi hizo Juni 3, 2025,TFS imekaribisha Maafisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Iringa katika Shamba la Miti la Sao Hill kwa ajili ya kutoa elimu kwa wahifadhi kuhusu namna ya kuepuka na kupambana na rushwa, sambamba na kuimarisha maadili ya utumishi wa umma.

Akizungumza katika mafunzo hayo,Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Iringa, Bw. Victor Swella,* alisema elimu hiyo inalenga kuwakumbusha watumishi kuhusu wajibu wao kwa umma na kuhimiza matumizi sahihi ya madaraka waliyopewa ili kuimarisha uwajibikaji na kuondoa mianya ya rushwa.

“Kila mtumishi wa umma anapaswa kutumia madaraka aliyopewa kwa kufuata taratibu, kanuni na sheria."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news