Rais Dkt.Samia atunukiwa tuzo maalum ya Power of 100 Women Award

DAR-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Julai 8,2025 Ikulu jijini Dar Es Salaam amepokea Tuzo Maalum ya Power of 100 Women Award kutoka kwa Uongozi wa Access Bank Group ambapo amekabidhiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Access Tanzania,ndugu Protase Ishengoma.
Tuzo hii ambayo hutolewa kila baada ya miaka mitano inalenga kutambua na kusherehekea wanawake wa Kiafrika wanaotoa michango ya mageuzi kwa mataifa na jamii zao, kuhamasisha na kuhimiza kizazi kijacho cha viongozi Wanawake katika bara zima la Afrika.

Pia kupaza sauti za Wanawake katika kuleta maendeleo endelevu ya Kiuchumi na kijamii barani Afrika.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Tuzo Maalum ya ‘Power of 100 Women Award mara baada ya kukabidhiwa Ikulu Jijini Dar es Salaam 08 Julai, 2025.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news