Wakuu wa Mamlaka za Kupambana na Rushwa Afrika waadhimisha Siku ya Kupambana na Rushwa barani Afrika 2025

ALGIERS-Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), Bw. Crispin Francis Chalamila, ameungana na Wakuu wa Mamlaka za Kupambana na Rushwa barani Afrika, kuadhimisha Siku ya Kupambana na Rushwa inayoadhimishwa mjini Algiers nchini Algeria.
Wakuu hawa ambao wako Algiers, wanashiriki maadhimisho haya kupitia 'Associstion of African Anti - Corruption Authorities - AAACA', ambao pamoja na mambo mengine watakuwa na Mkutano Mkuu wa 7 wa Mwaka wa Shirikisho hilo,Julai 21 na 22, 2025.

Maadhimisho haya yanafanyika nchini Algeria katika ukumbi wa 'International Conference Center - Abdelatif Rahal, Algiers - Algeria' na kuhudhuriwa na washiriki takriban 250 wakiwemo viongozi kutoka nchi 28 za Afrika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news