Banda la NHC lavutia wengi CEOs Forum

ARUSHA-Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limeendelea kuvutia washiriki wa Kongamano la Wenyeviti wa Bodi na Wakurugenzi wa Taasisi za Umma linaloendelea katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (AICC) jijini Arusha.
Miongoni mwa viongozi waliotembelea banda la NHC ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Joyce Mapunjo, ambapo alipata fursa ya kujionea huduma, mafanikio na fursa mbalimbali zinazotolewa na Shirika.

Kongamano hilo, ambalo linatarajiwa kufunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango, limewaleta pamoja viongozi wa mashirika ya umma, wenyeviti wa bodi na watunga sera kwa lengo la kujadili mbinu za kuimarisha taasisi za umma na mchango wake katika maendeleo ya Taifa.
Kupitia ushiriki wake, NHC inaendelea kuonesha dhamira ya kuimarisha ushirikiano na taasisi nyingine za kimkakati, sambamba na kuongeza ubunifu, ufanisi na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news