Makamu wa Rais Dkt.Mpango atembelea banda la NHC kongamano la CEOs Forum

ARUSHA-Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango ametembelea banda la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika Kongamano la Wenyeviti wa Bodi na Wakurugenzi wa Taasisi za Umma linaloendelea katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (AICC) jijini Arusha.
Katika banda hilo, Mheshimiwa Dkt.Mpango amepokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Bw.Hamad Abdallah ambaye amemuelezea kuhusu huduma na miradi mbalimbali inayotekelezwa na shirika ikiwemo ile ya kimkakati nchini.
Dkt.Mpango anafungua kongamano hilo ambalo limewaleta pamoja viongozi wa mashirika ya umma, wenyeviti wa bodi na watunga sera, kwa lengo la kujadili mbinu za kuimarisha taasisi za umma na mchango wake katika maendeleo ya Taifa.
Kupitia ushiriki wake, NHC inalenga kuimarisha ushirikiano na taasisi nyingine za umma pamoja na wadau wa sekta ya fedha, ili kuongeza ubunifu, ufanisi na upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news