Mawaziri,wanajeshi wafariki katika ajali ya ndege

ACCRA-Mawaziri wa Ulinzi na Mazingira wa Ghana wamefariki katika ajali ya Helikopta ya Kijeshi katika eneo la kati la Ashanti, pamoja na watu wengine sita.
Julius Debrah ambaye ni Mkuu wa Majeshi amewaeleza waandishi wa habari kuwa,Waziri wa Ulinzi Edward Omane Boamah na Waziri wa Mazingira, Sayansi na Teknolojia,Ibrahim Murtala Muhammed (50) wamefariki katika ajali hiyo ambayo amesema ni pigo kubwa kwa Taifa hilo.

Helikopta hiyo imeondoka katika mji mkuu wa Accra, saa 09:12 kwa saa za huko na ilikuwa inaelekea katika mji wa uchimbaji dhahabu wa Obuasi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news