TMDA yabaini uwepo wa Dettol za maji bandia katika soko

DAR-Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imetoa taarifa kwa umma kuhusu kubaini uwepo wa Dettol za maji bandia zenye ujazo tofauti, ambazo zinatengenezwa kinyume cha sheria.
Uhalifu huu ulibainika baada ya taarifa za kiintelijensia zilizopelekea ukaguzi wa pamoja na Jeshi la Polisi katika nyumba ya kulala wageni ya New Kishimbe Lodge, iliyopo Mtaa wa Namanga, Kahama Mjini Mkoa wa Shinyanga.

Katika ukaguzi huo, TMDA na Polisi walikuta malighafi mbalimbali zikiwemo chupa tupu, lebo, rangi, na kemikali, katika chumba walichokuwa wakiishi watuhumiwa wawili kutoka nchi jirani.

Watuhumiwa hao wamefikishwa katika vyombo vya usalama kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news