Wanafunzi wa shule mbalimbali watembelea Makumbusho ya Benki Kuu ya Tanzania

DAR-Wanafunzi kutoka shule mbalimbali nchini wametembelea Makumbusho ya Benki Kuu ya Tanzania iliyopo katika ofisi za Benki Kuu (BoT) jijini Dar es Salaam.
Katika ziara hiyo, wanafunzi hao walipata fursa ya kujifunza kuhusu historia ya fedha ya Tanzania,mabadiliko ya majukumu ya Benki Kuu tangu kuanzishwa kwake hadi sasa pamoja na mageuzi mbalimbali yaliyofanyika katika sekta ya fedha nchini.
Makumbusho hii itakuwa wazi siku za Jumatatu, Jumatano na Ijumaa kuanzia saa 3:00 Asubuhi hadi saa 9:00 Alasiri. Benki Kuu inawakaribisha wananchi wanaopenda kutembelea makumbusho hii kuwasilisha maombi yao kupitia barua pepe C_DEPT_STAFF@bot.go.tz

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news