Mhandisi Zena Ahmed Said aipongeza BoT kwa kuendelea kuelimisha umma masuala ya fedha na uchumi

GEITA-Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhandisi Zena Ahmed Said, amepongeza Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa jitihada zake za kuelimisha umma kuhusu masuala ya fedha na uchumi kupitia ushiriki wake katika Maonesho ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea mkoani Geita.
Mhandisi Zena alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la BoT, ambapo alipokelewa na Meneja wa Idara ya Mawasiliano BoT, Bi. Victoria Msina. Katika maelezo yake, Bi. Msina alieleza kwa kina huduma zinazotolewa na wataalamu wa BoT kwa wananchi wanaotembelea banda hilo.
Elimu inayotolewa na Benki Kuu katika Maonesho haya ni chachu ya kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu namna ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya kiuchumi na kifedha kwa manufaa ya taifa zima.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news