Rais Dkt.Mwinyi aongoza viongozi na mamia ya wananchi katika maziko ya kaka yake Abbas Ali Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewaongoza viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na mamia ya wananchi katika maziko ya kaka yake, marehemu Abbas Ali Mwinyi, aliyefariki jana.
Maziko hayo yamefanyika leo tarehe 26 Septemba 2025, Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Mapema, Dkt. Mwinyi alijumuika na waumini wa dini ya Kiislamu, ndugu, jamaa na marafiki kwa Sala ya Ijumaa pamoja na Sala ya kumsalia marehemu katika Msikiti wa Jamia Zinjibar, Mazizini, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news