RC Shigela atembelea banda la BoT katika Maonesho ya Teknolojia ya Madini

GEITA-Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Martine Shigela ametembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwenye Maonesho ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea katika viwanja vya EPZ Bombambili, mkoani Geita. Maonesho hayo yanafanyika kuanzia Septemba 18 hadi 28, 2025.
Katika ziara yake, Mhe. Shigela alipatiwa maelezo kuhusu ushiriki wa Benki Kuu kwenye maonesho hayo, ambao unalenga zaidi kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake ya msingi katika kusimamia uchumi wa taifa. Miongoni mwa majukumu hayo ni kuhifadhi akiba ya fedha za kigeni na dhahabu.
Hadi kufikia Agosti 2025, Benki Kuu ilikuwa imenunua jumla ya tani 9.165 za dhahabu zenye thamani ya takribani Dola za Marekani milioni 1,015.98, hatua inayochangia kuimarisha hifadhi ya taifa na kudumisha uthabiti wa uchumi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news