Dkt.Mwamba aongoza Ujumbe wa Tanzania katika kikao cha IFC

WASHINGTON-Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, aliongoza Ujumbe wa Tanzania katika kikao na IFC - International Finance Corporation kilichokuwa chini ya Mkurugenzi wa Taasisi hiyo anayesimamia Kanda ya Afrika Mashariki, Bi. Mary Peschka ambapo pamoja na mambo mengine, walijadili kuhusu ushirikiano uliopo kati ya taasisi hiyo iliyo chini ya Benki ya Dunia na Tanzania.
Miongoni mwa masuala muhimu yaliyojadiliwa ni pamoja na taasisi hiyo kushirikiana na Tanzania kutekeleza programu mpya ya kuendeleza kilimo biashara (AgroConnect), kuendeleza nishati safi, na ya gharama nafuu kusaidia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendelo 2050, kuendeleza sekta binafsi na masuala ya fedha kwa ujumla.
Kikao hicho kilihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Dkt. Elsie Kanza, Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA Leonard Mkude, Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Japhet Justine, Kamishna Msaidizi kutoka Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Fedha, Bw. Robert Mtengule, Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania, Bw. Nathan Belete na viongozi wengine waandamizi wa Serikali na Benki ya Dunia.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news