Filipe Pedro ndiye Kocha Msaidizi wa Yanga SC

NA DIRAMAKINI

KLABU ya Young Africans Sports Club (Yanga SC) imemteua Filipe Duarte da Silva Pedro raia wa Ureno kuwa Kocha Msaidizi ambaye atasaidiana na Kocha Mkuu wa klabu hiyo,Pedro Goncalves.
Ujio wa kocha huyo unalenga kuimarisha mbinu za mafunzo, maendeleo ya wachezaji, na mikakati ya kiufundi ya timu katika mashindano ya ndani na nje ya nchi.

Filipe Pedro mwenye umri wa miaka 38 ana leseni ya UEFA Daraja la A na ana uzoefu mkubwa katika klabu za vijana na timu za wakubwa.

Kabla ya kujiunga na Yanga SC, aliwahi kuwa kocha wa timu ya vijana ya Sporting Clube de Portugal (U19), moja ya akademi bora zaidi barani Ulaya inayojulikana kwa kukuza wachezaji nyota duniani.

Kwenye majukumu yake mapya, Pedro atafanya kazi kwa karibu na kocha mkuu wa Yanga SC, akijikita katika kuimarisha uchambuzi wa mchezo na wapinzani,kuandaa programu za mafunzo ya wachezaji kulingana na viwango vya kimataifa.

Pia,kutumia teknolojia ya kisasa ya michezo katika upangaji na tathmini ya mazoezi, kocha huyo anatajwa kuwa mwalimu mwenye ujuzi na nidhamu ya hali ya juu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news