KATIBU Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri, ametembelea mitambo ya uzalishaji maji ya Ruvu Juu na Ruvu Chini mkoani Pwani, na kuitaka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kuongeza kasi ya usambazaji maji ili kuhakikisha huduma hiyo muhimu inawafikia wananchi wote kwa wakati.
Katika ziara hiyo, Mhandisi Mwajuma aliambatana na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Mkama Bwire, pamoja na Menejimenti ya Mamlaka hiyo. Lengo kuu la ziara lilikuwa ni kufuatilia hali ya uzalishaji wa maji na hatua za usambazaji katika maeneo ya Dar es Salaam na Pwani.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo














