Magazeti leo Oktoba 26,2025

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri, ametembelea mitambo ya uzalishaji maji ya Ruvu Juu na Ruvu Chini mkoani Pwani, na kuitaka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kuongeza kasi ya usambazaji maji ili kuhakikisha huduma hiyo muhimu inawafikia wananchi wote kwa wakati.
Katika ziara hiyo, Mhandisi Mwajuma aliambatana na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Mkama Bwire, pamoja na Menejimenti ya Mamlaka hiyo. Lengo kuu la ziara lilikuwa ni kufuatilia hali ya uzalishaji wa maji na hatua za usambazaji katika maeneo ya Dar es Salaam na Pwani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news