TMA yatoa angalizo kwa wakazi wa Pwani kuhusu kimbunga CHENGE

NA DIRAMAKINI

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya hali ya hewa kwa wakazi wa maeneo ya pwani na watumiaji wa bahari, ikiwataka kuwa makini na kufuatilia taarifa za hali ya hewa kutokana na kuendelea kusogea kwa Kimbunga CHENGE kuelekea magharibi zaidi mwa Bahari ya Hindi ulipo ukanda wa pwani wa Tanzania.
Hadi kufikia asubuhi ya leo Jumamosi, kimbunga hicho kilikuwa takribani kilomita 1,280 mashariki mwa pwani ya Kisiwa cha Mafia.

Kwa mujibu wa taarifa ya TMA, mfumo huo wa hewa unatarajiwa kupungua nguvu hatua kwa hatua kadri unavyokaribia mwambao wa Tanzania.

TMA imewahimiza wakazi wa maeneo hayo na watumiaji wa bahari kuendelea kufuatilia taarifa na utabiri wa hali ya hewa kila wakati.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news