Mfanyabiashara jela miaka mitatu kwa rushwa na magendo Missenyi

KAGERA-Mahakama ya Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera chini ya Hakimu Mfawidhi Mheshimiwa Yohana Muyombo leo Oktoba 17,2025 imemhukumu kifungo cha miaka mitatu jela bila faini mfanyabiashara Martine Muyobya Tabura.
Picha na mtandao.


Katika kesi ya jinai namba CC 25329/2025, Muyobya alishtakiwa kwa kosa la kukiuka kifungu cha 15(1)(a) na (2) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Sura ya 329, Marejeo ya Mwaka 2023.

Mahakama ilielezwa kuwa,kati ya tarehe 11 hadi 25 Julai, 2025, mshtakiwa akiwa mfanyabiashara, aliingiza vifaa vya muziki vyenye thamani ya shilingi 9,285,714 kutoka nchini Uganda kwa njia za magendo bila kulipa kodi stahiki ya serikali.

Kitendo hicho kilisababisha hasara kwa serikali ya jumla ya shilingi 3,958,118 ikiwa ni kodi iliyopaswa kulipwa.

Shauri hilo liliendeshwa na waendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Bw. Sospeter Joseph na Bw. William Musso, ambao waliwasilisha ushahidi uliowezesha Mahakama kutoa hukumu hiyo kali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news