Rais Dkt.Mwinyi atangaza Oktoba 29,2025 kuwa siku maalum ya mapumziko kwa wananchi wote Zanzibar

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi ametangaza Jumatano, tarehe 29 Oktoba, 2025 kuwa siku maalum ya mapumziko kwa wananchi wote wa Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Taarifa hiyo imetolewa leo Oktoba 23, 2025, ambapo Rais Dkt.Mwinyi amesema, uamuzi huo unalenga kuwapa wananchi wote waliokidhi vigezo nafasi ya kushiriki kikamilifu katika zoezi la kupiga kura kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Aidha, Rais Dkt.Mwinyi amewasihi wananchi wote kufuata miongozo na maelekezo yatakayotolewa na Tume Huru ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani, utulivu na nidhamu, kama ilivyo desturi ya Zanzibar.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news